Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Machi, 2021

SABABU ZA KUKU KULA MAYAI

Picha
  Kuku hula mayai kwa sababu nyingi sana ambazo zingine au zote zinaweza kuzuilika, 1.Tabia yao tu- Hapa utakuta ndo uzao wao wanatabia ya kula mayai hivyo kuku hufanya muendelezo wa kula mayai, 2.Kuto kupata chakula cha kutosha- Hii ni moja ya sababu kubwa kabisa inayo pelekea kuku kula mayai. 3.Kukosa madini joto- Hii inaweza kuwa ndo sababu kuu ya kwa nini kuku wanakula mayai, kuku wakikosa madini joto ni lazima wale mayai na hata kulana wao wenyewe, . 4.Lishe mbaya chakula unacho wapatia huja changanya na  madini yeyote 5.Nafasi ndogo ambayo ita sababisha msongamano na kupelekea kudonoana  au kula mayai. 6.Kukosa shughuli kama za kuparua au kula chakula 7.Ukoo/aina au asili ya kuku anayo tokea NAMNA YA KUZUIA KUKU KUDONOANA AU KULA MAYAI 1.Chakula cha kutosha ni muhimu sana, ili kuwafanya wasitake kula mayai ili kushiba. 2.Maji yakusanywe mara tu anapo taga na usiyaache muda mrefu bandani. 3.Sehemu ya kutagia iwe na giza la kutosha ili kufanya kuku ashindwe kuona yai ...

NDUI YA KUKU(FOWL POX)

Picha
Ndui ni ugonjwa unaosababishwa na virusi ambavyo hushambulia zaidi kuku, jamii ya bata na aina nyingi ya ndege pori. Kuku na ndege wa umri tofauti wote huweza kushambuliwa na sehemu zinazoathirika zaidi ni zile zisizo na manyoya. Virusi vinaweza kuishi katika mazingira kwa muda mrefu. Jinsi Ugonjwa Unavyoenea . -Chanzo cha maambukizi ni vifaa/vyombo vya shambani vilivyochafuliwa na kinyesi cha kuku wagonjwa na wenye vimelea.  -Maambukizi pia kuenea kupitia wadudu wanaouma kama chawa, kupe, nzi weusi na mbu. -Maambukizi pia kuenea kupitia majeraha wanayoyapata kuku wanapopigana na kukwaruzana au kugusana Maambukizi kupitia mfumo wa hewa na chakula. Dalili Kuku aliyevimba macho Ugonjwa unapoathiri ngozi hutokea vipele vikubwa vya rangi ya kijivu au kahawia kwenye upanga, undu, macho na mdomoni au sehemu zisizo na manyoya. Ugonjwa unapoathiri sehemu laini za mwili, mabaka madogo meupe hutokea kwenye kona za mdomo, kuzunguka ulimi, ndani ya mdomo na kwenye koo. Malengelenge kwenye kish...

MAFUA MAKALI (INFECTIOUS CORYZA)

Picha
Huu ni ugonjwa amba una shambulia kuku na ndege waporini , nauna wapata hasa kuku wa lika lolote. Ugonjwa huu huanza taratibu kwa kuku mmoja na kwenda kwa kuku wengine/mwingine endapo usipo udhibiti mapema na husababisha machokutoa machozi     Ugonjwa huu hushambulia sana mfumo wa hewa na kupelekea nuonekana kwa dalili zifuatazo:- ·        Kuku kukoroma ·        Makamasi mazito kutoka puani. ·        Kuku Kupiga chafya sana. ·        Uso kuvimba hasa maeneo ya macho. ·        Vifo vingi bandani kila siku NINI KIFANYIKE ·        Hakikisha banda la kuku lina ruhusu hewa ya kuingia na kutoka ·        Hakikisha unapo weka Maranda yasiwe yaliyo toka mashineni ·        Hakikisha banda la kuku wa dogo lisiwe mwelekeo wa k...

MDONDO/KIDERI(NEWCASTLE DISEASE)

Picha
MAGONJWA YA KUKU Ugonjwa huu huwapata jamii ya ndege(kuku) wakubwa na wadogo na ni miongoni mwa magonjwa hatari ambayo huambukizwa na vimelea aina ya Paramyxovirus Dalili za mdondo/kideri 1.Vifo vya ghafla 2.Kukosa hamu ya kula 3.kuharisha kinyesi cheupe na kijani. 4.kuhema kwa shida. 5.Kutoa udenda mdomoni 6.Kuhema kwa shida 7.Kukakamaa viungo au kupooza mabawa miguu na shingo pia 8.Kupunguza kasi ya utagaji 9.Vifo hutokea kwa kasi ya ugonjwa na hufikia asilimia100% Jinsi ugonjwa unavyo enea Ugonjwa wa Mdondo / kideri(Newcastle Disease) huenea au huenezwa kwa njia mbalimbali kama zifuatazo:-   ·          - Kwapatia maji yenye maambukizi ·          - Kula chakula kilicho liwa na kuku mwenye maambukizi ·          - Kugusana kwa kuku mwenye ugonjwa na asiye naugonjwa. ·          - Hewa yenye maambukizi   ya magonjwa ·          - Uingiaji wa watu ka...